WASANII BONGO MOVIES WAUKIMBIA MWALIKO WA BUNGE KUSIKILIZA MSWADA WAO

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa
Waigizaji wa filamu nchini leo wanadaiwa kukwepa mwaliko bungeni walikotakiwa kwenda muswada wa marekebisho kwenye sheria ya Filamu na Michezo ya Kuigiza (1976).
Kupitia Twitter muigizaji mrembo, Yobnesh Yussuph maarufu kama Batuli, amesema amefuatilia mjadala huo kupitia TV lakini amesikitishwa kubaini kuwa wapo wasanii walioalikwa lakini hawakwenda bungeni.
“Yes nimefuatilia bunge ila cha kusikitisha ni wasanii waliopewa mwaliko halafu hawajaudhuria,” aliandika Batulli.
“Nalaani sana kitendo cha walioalikwa kutokufika bungeni kwenye hoja nyeti kama hii nikiwajua sitawanyamazia,” aliongeza.
Naye Lulu alijibu: Hatujichukulii serious ndo mana hatuchukuliwi serious pia..unaachaje kuhudhuria mwaliko unaokuhusu halafu umealikwa? Ndo tatizo la kutokuwa na umoja, haya tutaendelea kulia tu.”

Source: Times Fm 
_________

 Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo na Makampuni Bonyeza HAPA

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad