Msanii Rich Movoko Amkana Mrembo Gigy Money 'Sikumbuki Hata Kukutana na Gigy Money Wala Kutoka Nae Kimapenzi Sinaga Upumbavu Huo'

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa
 Gigy Money na Rich Mavoko....
Msanii Rich Mavoko amekanusha taarifa za kuwahi kuwa na mahusiano na video queen Gigy Money, ambaye alisema alishawahi kuwa naye akiwa kidato cha pili.

Akiongea na East Africa Radio Mavoko amesema taarifa hizo si za kweli, na hakumbuki hata kuwahi kukutana naye mrembo huyo, achilia mbali kuwa na mahusiano naye.
“Mi sijawahi kutoka naye, hata siku moja sijawahi, sina urafiki naye na wala sijawahi kuongea naye, sijui kama alishawahi kukutana na mimi, sijaweka kichwani kama nishawahi kukutana nae sikumbuki.

Mavoko ameendelea kusema "Sijawahi kuwa na skendo za kipumbavu, mi ni mtu ambaye sijawahi kuwa na upumbavu kama huo, kwanza mi mwenyewe nashangaa unajua kila kitu, sijawahi kutoka naye sijui mwenyewe anafikiria nini, siwezi kujua, siwezi kutambua, sijawahi kuelewa nini kilichompelekea hivyo”, alisema Richi Mavoko.

Hivi Karibuni video queen huyo alisema alishawahi kuwa na mahusiano na msanii huyo wakati yupo kidato cha pili, kitu ambacho ni kinyume na sheria za nchi na hakifai kwa mtu ambaye ni kioo cha jamii.
_________

 Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo na Makampuni Bonyeza HAPA

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad