Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa
Ishu nzima ilianza baada ya mwandishi wetu kupata ubuyu kutoka kwa mmoja wa watu wa karibu wa Lulu Diva kuwa anamhofia Gigy Money kumfunika katika gemu wanalofanya.
Baada ya mwandishi wetu kupewa ubuyu huo alimwendea hewani Lulu, aliposomewa madai hayo mwanadada huyo alisema;
“Nani kakwambia hivyo? Siwezi kumhofia Gigy kwenye kile ninachokifanya, hana kitu chochote cha kunifanya nimhofie maana ni mtu wa kawaida sana kwangu.”
Kwa upande wa Gigy alipotafutwa alisema; “Siwezi kupigizana kelele na huyo demu, anatafuta kiki kupitia kwangu lakini hawezi kuipata hata kwa dawa, haniwezi kwa kila kitu, akajipange sana na akae akijua simuogopi.”
Global Publishers
Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo na Makampuni Bonyeza HAPA
LILA NA FILA HAZITANGAMANI MPO HAPO NYIE MABINTI WA SHOBO?
ReplyDelete