BSS Kuna Uchawi Gani? Mbona Wengi Hawafanikiwi?

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa
Waungwana leo kwenye pita pita yangu nilikutana na miongoni mwa washiriki wa BSS aliyekuwa miongoni mwa waliofanya vizuri (jina kapuni) akiwa kachoka sana mpaka nikamuonea huruma, sasa nikawa najiuliza hivi hili shindano lina manufaa gani? Kwa nini washiriki wengi hawafanikiwi na majina yao hufifia baada ya muda mfupi?

Tuchukulie mfano mtu kama Jumanne Idd mpaka leo hajulikani halipo alkadharika Walter Chilambo, Kayumba , AngelMarry Kato , Steven Lupenza, Nasibu Fonabo nk ni miongoni mwa vijana ambao wana uwezo mkubwa sana wa kuimba lakini cha ajabu hawafanikiwi kulinganisha na washiriki wengine kama vile Harmonize ingawa alitoka mapema na kuonekana si chochote leo hii katudhihirishia kwamba yeye ana uwezo gani....

By Hance mtanashati


Jibu la Mdau

Kwanza ni jambo la kujiridhisha kuwa si BSS tuu bali hata huko nje shows kama za the voice, SA idols, xfactors, na Got talents za nchi nyingi, ni watu wachache sana walio shinda mashindano ya aina hii wame make ki muzik.
Kwanini!!?
1. Lengo la mashindano, waandaji huwa wanaandaa kwa ajili ya faida yao na kupata wadhamini, na mara nyingi wakisha maliza shindano hawawekezi kwa nguvu kubwa kwani kuna shindano la mwakani inabidi waandae tena, hawana time na wewe
Pia washindanaji lengo lao kubwa zaidi ni kupata yale mamilioni tuu, wakisha pewa kuna msemo unasema easy come easy go
2. Mashabiki wa mashindano, askudanganye mtu, watanzania wanao fuatilia BSS ni chini ya milioni 10, wanao piga kura ni chini ya laki moja, kwa hiyo kama msanii ukishinda unakuwa hujapata fan base kubwa bado isipo kuwa ki portion kidooogoo cha wale walio angalia na wakajisumbua hata kupiga kura,,na wengi wanai piga kura huwa wanaanza kwanza kukuonea huruma ya kimaisha mfano unakumbuka Jumaanne Idd kwa hiyo Raymond akitoa wimbo mmoja uka hit anapata fan base kubwa kuliko wewe mshindi
3. Mziki ni zaidi ya kukopi nyimbo za watu, angalia yule mshindi wa mwaka jana kayumba alishnda kwa kuimba imba taarab za kina isha mashauz sasa je akitoka BSS ana uweza huo mziki!!? Mpaka yeye mwenyewe hajui afanyeje yaani

*Sababu ni nyingi lakini kikubwa ni wasanii wajiamini wahue uwezo wao ni zaid ya kuimba BSS, ndio maana mara nyingi unakuta wanao fanikiwa ndio wale walio shika u tano, au ukumi, kwa kuwa it takes more than to win BSS ili kuwa msanii

By Ice Man 3D

_________

 Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo na Makampuni Bonyeza HAPA

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. majibu ya mdau nimeyaona mbali na majibu ya kulidhisha lakini bado kuna swali la kujiuliza kwanini wale wanaoibuka kidedea kwenye mashindano haya ndo awafanyi vizuri...lakini wale wa asante kushiriki ndo wamekuwa wakifanya vizuri kwenye muziki..mfano mzuri harmonize, kala jeremiah, baby madaha hawa wameonesha wanakipaji tofauti na majaji walivyowajaji..mimi nadhan kwenye sababu nying na kupangwa kwa matokeo ni sababu mojawapo

    ReplyDelete
  2. wewe mdau hapo juu umeaddika kuwa watu waliofanikiwa kuwa Babe Madaha ni mmoja wao hivi wewe huwa unasoma magazeti, Baby Madaha aliandikwa sana kwenye magazeti siku za nyuma sababu alikuwa anataka kujiuza kwa mfanya biashara, yeye mwenyewe Baby Madaha aliomba msamaha kwa watanzania asamehewe kuwa hatorudia tena, kama angekuwa amefanikiwa kwenye mziki asingejiabisha namna hiyo kwenye biashara ya kujiuza na kama angefanikiwa vizuri kwenye mziki wala asingekuwa na hata mawazo ya kujiza

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad