TATU Bora Mchezaji Bora Afrika Zatoka

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa

Mshambuliaji raia wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang, mshambuliaji na winga wa Algeria Riyad Mahrez na winga wa Senegal  Sadio Mané wameingia kwenye orodha ya wachezaji wattau bora wa tuzo ya mchezaji bora wa Afrika.

Wachezaji hao watatu wamefika hatua hiyo baada ya kupigiwa kura na makocha na wakurugenzi wa ufundi wa vyama vya soka vilivyokuwa chini ya  CAF, kamati za vyombo vya habari, kamati za soka na ufundi na wataalamu wa habari. Mohamed Salah na Slimani hawajafanikiwa kuingia katika hatua hii.

Kwa mchezaji bora wa Afrika kwa ligi za ndani, golikipa wa Uganda Dennis Onyango na Mzimbabwe Khama Billiat na mchezaji wa Zambia kiungo Rainford Kalaba wameingia.

TWashindi watatangazwa kwenye tuz hizo maarufu kama Glo-CAF Awards Gala siku ya Alhamis, 5 January 2017 jijini Abuja, Nigeria.

 

Mchezaji bora wa Afrika

Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon & Borussia Dortmund)

Riyad Mahrez (Algeria & Leicester City)

Sadio Mané (Senegal & Liverpool)

 

Mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani.

Denis Onyango (Uganda & Mamelodi Sundowns)

Khama Billiat (Zimbabwe & Mamelodi Sundowns)

Rainford Kalaba (Zambia & TP Mazembe)
_________

 Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo na Makampuni Bonyeza HAPA

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad