Baada ya Okwi Kuvunja Mkataba Denmark,Simba Wamfanyia Mapango Aje Kucheza Mechi ya Yanga..!!

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa

UONGOZI wa Simba umesema unafanya mpango wa kumrejesha kikosini mshambuliaji wake wa zamani Emmanuel Okwi aliyevunja mkataba na klabu ya Sonderjyske ya Denmark.

Taarifa za kwenye mtandao wa klabu hiyo juzi ziliandika kwamba Okwi amefikia makubaliano ya kuvunja mkataba baada ya kukosa nafasi ya kucheza kwenye kikosi hicho.

Jana jioni Ofisa habari wa Simba, Haji Manara aliandika kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii: “Kocha Omog (Joseph- kocha mkuu wa Simba) ikimpendeza, Emmanuel Okwinho (Okwi) dimbani Feb 18, hiyo ndio habari mpasuko, ukinuna ongeza limao,”.

Simba inatarajia kucheza na Yanga katika mechi ya raundi ya pili ya Ligi Kuu baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika mechi ya kwanza.

Alipoulizwa  kuhusu taarifa hizo, Manara alikiri kuwa uongozi wake uko kwenye mchakato wa kumnasa mchezaji huyo na ikiwezekana atumike kwenye mechi zilizosalia za Ligi Kuu.

“Ni kweli tutamsajili kama mchezaji huru,” alisema.

Hata hivyo, tayari dirisha dogo la usajili kwa klabu za ligi limeshafungwa mpaka msimu ujao. Akilizungumzia hilo, ofisa habari wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas alisema Simba haiwezi kumtumia Okwi kwa sababu dirisha la usajili limeshafungwa.

“Ingewezekana kama usajili wa dirisha dogo ungekuwa haujafungwa, lakini dirisha limeshafungwa hivyo kama wanataka kumtumia, wasubiri mpaka usajili mwingine,” alisema.

Wakati wa usajili wa dirisha dogo Desemba mwaka jana Simba ilitaka kumsajili mshambuliaji huyo Mganda lakini ilishindwa baada ya klabu ya Sonderjyske kutaka ilipwe karibu sh milioni 240.

Hasimu wa Simba, Yanga pia ilijaribu kutaka kusajili mshambuliaji mwingine ili ashindane na Donald Ngoma baada ya kudaiwa kugoma kucheza kwenye mechi za kombe la Mapinduzi lakini ilishindikana kwa vile dirisha la usajili lilishafungwa.

Sonderjyske ilimsajili Okwi Julai 2015 kutoka Simba kwa mkataba wa miaka mitano uliotakiwa kumalizika mwaka 2020 ambapo tangu amesajiliwa Okwi alicheza mechi nne tu za Ligi Kuu ya Denmark na mbili za kombe la DBU ambapo alifunga mabao mawili.

Simba pia iliwahi kumuuza Okwi Etoile du Sahel ya Tunisia mwaka 2013 kwa dola za Marekani 300,000 kabla ya kusajiliwa na Yanga alipocheza kwa muda mfupi na kurejea Simba.

Okwi ni mshambuliaji kipenzi cha wanasimba kutokana na mafanikio aliyoipatia timu hiyo ambapo jana baada ya Manara kuweka suala lake kwenye mitandao ya kijamii, karibu mashabiki wengi wa soka walikuwa wakimzungumzia.
_________

 Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo na Makampuni Bonyeza HAPA

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mmmmh hawa viongozi wa simba hawajiulizi kwa nini Sonderjyske hawakuwa wanamtumia?Hivi inawezekana mchezaji mzuri na nidhamu safi asipate namba kweli?Tatizo la simba Viongozi ndio wanamtaka Okwi,tunarudi tena kulekule kwa kutaka kumfunga Yanga tu ubingwa tuusikie kwa wenzetu,sio vyema kabisa.Mna uhakika gani kama Okwi yule ndio Okwi wa sasa ukizingatia alikuwa hachezi?Tutaendelea kutafuta mchawi wakati mchawi tunatembea nae,tuna wimbo yanga wanabebwa wakati ukiangalia makosa yanayowafanya yanga waonekane kubebwa na simba yapo.Wachezaji wa Yanga na viongozi wao kwa sasa wametulia,wako kimya hadi raha,angalia kwetu sasa mipasho utadhani waimba taarabu,hakuna nidhamu kabisa.Fanyeni kama wasomi bhana,mashabiki tumeumia vya kutosha.

    ReplyDelete
  2. WA KAZI GANI?HIVI HAKUNA MWINGINE MPAKA MNARUDISHA OKWI MARA MBILI TATU MSIMBAZI?

    ReplyDelete
  3. HAHAHAHAHA MMEKURUPUKA,HAWEZI KURUHUSIWA KUCHEZA USAJILI USHAFUNGWA AU KIGEZO GANI KITATUMIWA?BASI KAMA HIVYO NA WENGINE WARUHUSIWE KUSAJILI.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad