Staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson ‘Gwantwa’ yupo hatarini kukatwa mkono kutokana na jeraha la chupa alilolipata hivi karibuni.
Tukio la Aunt kupigwa chupa na mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Yvonne nje ya Club Bilicanas, Posta jijini Dar, lilitokea Agosti 26, mwaka huu wakati staa huyo alipokwenda kujiachia na mshosti zake.
Baada ya kupigwa chupa siku hiyo, Aunt alikimbizwa katika Hospitali ya Aga Khan lakini bahati mbaya alikosa daktari wa kumtibu hivyo akalazimika kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Dk. Mvungi, Kinondoni ambapo alishonwa nyuzi sita pamoja na dawa za kukausha kidonda.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Aunt ni muoga wa dawa na wakati kidonda kikiwa bado hakijapona vizuri aliacha kumeza dawa alizopewa.
Chanzo hicho kilisema tatizo la staa huyo kukatisha dozi lilisababisha kidonda kishindwe kupona na badala yake kikaanza kutengeneza usaha na taratibu mkono ukaanza kuoza.
“Mkono ulifikia hatua ukaanza kuoza kwani licha ya kushonwa lakini kilibadilika rangi ndipo alirudi hospitali.
Imeelezwa kuwa mapema wiki hii, Aunt alirudi tena katika Hospitali ya Dk. Mvungi na kusafishwa upya kidonda baada ya madaktari kugundua tatizo lilizidi kuongezeka.
Kwa mujibu wa nesi wa hospitali hiyo aliyeomba hifadhi ya jina lake, hali ya Aunt ilimshtua daktari, akamwambia aombe Mungu kwani kidonda kilichimbika sana na tatizo kama hilo huweza kusababisha mtu kukatwa mkono.
“Iligundulika mkono ulikuwa unaoza, daktari alimwambia amuombe Mungu kwani hatua iliyokuwa imefikia ni mbaya hivyo asipokuwa makini tatizo hilo litamfanya akatwe mkono,” alisema nesi huyo.
Aunt alipigwa chupa akigombania penzi la mwanaume na Yvone .
-Gpl & Aman
Akome umalaya
ReplyDeleteHuyo hata akipona haachi, ipo kwenye damu, kwani kabila gani vile????
ReplyDeleteMungu amsaidie jamn
ReplyDeleteMnyakyusa
ReplyDeletePole aunt, hii ndo dunia inavyozunguka. Mungu ukusaidie upone haraka ili imjue km yupo.
ReplyDeletewatu mna maneno jamani!!! eti kabila gani. dah kama huo ndo mkono wako kweli bas hali yako mbaya dada.pole ,haifai kumuombea mabaya tumuombee kwani kazi zake nzuri tu
ReplyDeleteMbona mkono kafafana na maini ya ngombe? doh!! pole dada
ReplyDeletemmh, hivi kama unahisi hujamaliza starehe zako unakimbilia nn kuolewa? fashion au? Uwoya nae majanga kila kukicha..kiruuu!! Aibu gn hii? Nakupenda sn aunty ila unaanza kunichefua kwa tabia zako. Upone haraka mamie
ReplyDeletepole sana aunt kazi ya mungu na utapona ila chamsingi kazana kumeza dawa usiache wala kupuuza i wish you all the best with lot's of love
ReplyDelete