MAPENZI YAMPONZA AUNT EZEKIEL, MKONO ALIOPIGWA CHUPA WAANZA KUOZA..!

Staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson ‘Gwantwa’ yupo hatarini kukatwa mkono kutokana na jeraha la chupa alilolipata hivi karibuni.

Tukio la Aunt kupigwa chupa na mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Yvonne nje ya Club Bilicanas, Posta jijini Dar, lilitokea Agosti 26, mwaka huu wakati staa huyo alipokwenda kujiachia na mshosti zake.

Baada ya kupigwa chupa siku hiyo, Aunt alikimbizwa katika Hospitali ya Aga Khan lakini bahati mbaya alikosa daktari wa kumtibu hivyo akalazimika kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Dk. Mvungi, Kinondoni ambapo alishonwa nyuzi sita pamoja na dawa za kukausha kidonda.

Kwa mujibu wa chanzo makini, Aunt ni muoga wa dawa na wakati kidonda kikiwa bado hakijapona vizuri aliacha kumeza dawa alizopewa.

Chanzo hicho kilisema tatizo la staa huyo kukatisha dozi lilisababisha kidonda kishindwe kupona na badala yake kikaanza kutengeneza usaha na taratibu mkono ukaanza kuoza.


“Mkono ulifikia hatua ukaanza kuoza kwani licha ya kushonwa lakini kilibadilika rangi ndipo alirudi hospitali.

Imeelezwa kuwa mapema wiki hii, Aunt alirudi tena katika Hospitali ya Dk. Mvungi na kusafishwa upya kidonda baada ya madaktari kugundua tatizo lilizidi kuongezeka.


Kwa mujibu wa nesi wa hospitali hiyo aliyeomba hifadhi ya jina lake, hali ya Aunt ilimshtua daktari, akamwambia aombe Mungu kwani kidonda kilichimbika sana na tatizo kama hilo huweza kusababisha mtu kukatwa mkono. 

“Iligundulika mkono ulikuwa unaoza, daktari alimwambia amuombe Mungu kwani hatua iliyokuwa imefikia ni mbaya hivyo asipokuwa makini tatizo hilo litamfanya akatwe mkono,” alisema nesi huyo.

Aunt alipigwa chupa akigombania  penzi  la  mwanaume  na  Yvone  .

-Gpl & Aman 
Tags

Post a Comment

9 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Huyo hata akipona haachi, ipo kwenye damu, kwani kabila gani vile????

    ReplyDelete
  2. Mungu amsaidie jamn

    ReplyDelete
  3. Pole aunt, hii ndo dunia inavyozunguka. Mungu ukusaidie upone haraka ili imjue km yupo.

    ReplyDelete
  4. watu mna maneno jamani!!! eti kabila gani. dah kama huo ndo mkono wako kweli bas hali yako mbaya dada.pole ,haifai kumuombea mabaya tumuombee kwani kazi zake nzuri tu

    ReplyDelete
  5. Mbona mkono kafafana na maini ya ngombe? doh!! pole dada

    ReplyDelete
  6. mmh, hivi kama unahisi hujamaliza starehe zako unakimbilia nn kuolewa? fashion au? Uwoya nae majanga kila kukicha..kiruuu!! Aibu gn hii? Nakupenda sn aunty ila unaanza kunichefua kwa tabia zako. Upone haraka mamie

    ReplyDelete
  7. pole sana aunt kazi ya mungu na utapona ila chamsingi kazana kumeza dawa usiache wala kupuuza i wish you all the best with lot's of love

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad