TANZANIA YAMKATAA BALOZI MPYA WA UJERUMANI

Dar es Salaam. Tanzania imemkataa Balozi mteule wa Ujerumani ambaye alitakiwa kuja kufanya kazi nchini.

Balozi huyo, Margit Hellwig-Boette alikuwa amemaliza muda wake nchini Kenya na alitakiwa kuja kuiwakilisha nchi yake Tanzania.

Balozi Hellwig-Boette alikaririwa na Gazeti la Standard la Kenya akieleza kuwa anajipanga kurudi kwao baada ya kukataliwa na Serikali ya Tanzania.

Alipoulizwa juu ya suala hilo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alikataa kuzungumzia suala hilo akisema: “Watu wa Wizara ya Mambo ya Nje ndio wanaoshughulika na hayo mambo, waulizeni.”

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mkumbwa Ally alisema wizara yake haijapata taarifa za kukataliwa kwa balozi huyo.

“Suala hilo linahusu ofisi ya Rais, mambo ya uteuzi ni ya Rais. Wizara ya Mambo ya Nje haina hiyo taarifa na hata kama ingekuwapo hiyo taarifa siyo ya `public’.

“Siyo taarifa ya umma kwa maana kwamba, mchakato wake ni wa siri na hayo mambo hayana kuuliza kwa nini. Ukileta jina la mtu unayetaka aje kuwa balozi likikataliwa, hakuna kuuliza eti ni kwa nini.

“Unachofanya ni kuleta jina jingine, hata Rais hapa akipeleka jina la mtu kwenye nchi nyingine lisiporudi, hakuna kuuliza unachofanya ni kuteua tu jina jingine,” alisema Mkumbwa.

Alikariri Kifungu cha Nne cha Azimio la Vienna ambacho kinaruhusu nchi kukataa balozi wa nchi nyingine bila ya kutoa sababu.

“Nchi inayopeleka balozi katika nchi nyingine inatakiwa kutoa jina mapema kwa nchi nyingine. Hata hivyo, nchi hiyo ina uwezo wa kumkubali au kukataa uteuzi,” kinaelekeza kifungu hicho.

Post a Comment

6 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Au wanahofia atakuwa Chadema maana balozi wa China ni CCM damu

    ReplyDelete
    Replies
    1. hahahahahahahahaha......hilo nalo neno mdau

      Delete
  2. hyo true kabs sapot inatoka hko

    ReplyDelete
  3. Huyo Mama kaharibu sana Kennya ndio maana Serikali yetu imemkataaa.Kama haujui uliza au kaaa kimya toa aComments kwenye mambo ingine sio Government

    ReplyDelete
  4. Nashukuru sana serekali ya kenya kwakuwatonya tanzania kuhusu kihelele alichokionyesha huyu balozi huko kenya nikweli anawezakukama huyu wa hapa kwetu huyu mchina. lakini walichokifanya wakenya ndicho huwa kinafanyo na makampuni mbalimbali kuwa ukiamua kuiacha kazi kwenye kampuni A kwenda B watapigiana simu nakulizana kama ulikuaunafanyaje kazi zako.hata vieti vya kuachakazi au barua huandikwa you can employ him on your on risk.m.ng.machimkenda

    ReplyDelete
  5. Sura yenyewe tu inaonyesha ana kimbele-front.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad