Imebainika:Serikali ilifanya Siri Ugonjwa wa Dengue

Ugonjwa wa homa ya dengue ambao umezidi kusambaa mkoani Dar es Salaam na kuathiri wilaya zake tatu za Temeke, Ilala na Kinondoni umezua hofu na taharuki kubwa kwa wananchi. Takwimu za Kitengo cha Utafiti wa Magonjwa cha Ifakara (IHI), kimeweka kambi katika Hospitali ya Mwananyamala hapa jijini kutafiti aina za homa zinaonyesha kuwa, kwa miezi miwili ya Machi na Aprili pekee, wagonjwa 85 walibainika kuwa na ugonjwa huo
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid.

Sisi tunadhani Serikali inastahili lawama kwa kutochukua hatua stahiki mapema kupambana na ugonjwa huo, ambao uliingia Dar es Salaam kwa mara ya kwanza mwaka 2010 na kuua wanafunzi kadhaa wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM). Juni mwaka jana, Wizara ya Afya ilithibitisha kuwapo kwa ugonjwa huo na Machi 26 mwaka huu, ilitoa taarifa kwa umma, ikisema wagonjwa 70 walikuwa wamebainika, 58 kati yao wakiwa Kinondoni, saba Temeke na watano Ilala.

Hata hivyo, wizara hiyo haikupaswa kuishia katika kutoa taarifa tu pasipo kuwaelimisha na kuwahamasisha wananchi nchi nzima kuhusu ugonjwa huo, namna ya kujikinga na nini cha kufanya iwapo wataambukizwa. Ulihitajika uwazi badala ya usiri, vinginevyo ugonjwa huo usingeenea kwa kasi tunayoishuhudia hivi sasa.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad