Messi Akubali Kubaki Barcelona, Sasa Amzidi Ronaldo Kwa Mkwanja

LIONEL Messi amekubali kusaini mkataba mpya katika klabu yake ya Barcelona na kuwa mchezaji anayelipwa zaidi duniani ambapo atakuwa anavuta mkwanja wa paundi milioni 16.3 kwa mwaka.
Baba yake, Jorge, amekutana na maofisa wa klabu Javier Faus na Antoni Rossich wiki iliyopita na kusaini mkataba wake wa 7 ndani ya klabu ya Barcelona.
Messi ambaye mwezi juni atafikisha miaka 27 baada ya kuongeza mkataba huo,  sasa atakaa Barcelona mpaka mwaka 2018.

Malipo atakayoyapata Messi kwa mwaka yamemfanya amuangushe nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo aliyekuwa anavuta paundi milioni 15 kwa mwaka mbali na marupurupu.
Tags

Post a Comment

6 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. sasa unafikiri mesi ni team gani inamtaka? Ht mkimtoa bure

    ReplyDelete
    Replies
    1. mbeya city inamtaka

      Delete
    2. Abajalo ya sinza leo kesho wanamtaka!

      Delete
  2. Safi sana messi. make sure leo unatupatia ubingwa wa laliga kwan uko njema.

    ReplyDelete
  3. wewe atletico anachukua io ipo wazi, haina mjadala... Messi kiwango kwisha c messi yule wa enzi izo

    ReplyDelete
  4. hahahaaa mdau, eti mbeya city inamtaka mesi...wkt ht tambwe amewashinda kumng'oa msimbazi

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad