Ndoa ya Kanye West na Kim Kardashian sasa Kufungwa Italia na si Ufaransa


Ripoti mpya zinadai kuwa harusi ya rapper Kanye West na mama wa mwanaye Kim Kardashian sasa itafanyika Italia na sio Paris, Ufaransa kama ilivyodhaniwa awali.

Entertainment Tonight imeripoti kuwa wageni waalikwa watakusanyika pamoja Paris, Ufaransa May 23 kwaajili ya chakula cha usiku ‘Pre wedding dinner’, na baada ya hapo couple hiyo itawasafirisha wageni wote kwa ndege binafsi tofauti kuwapeleka Florence, Italy ambako sherehe rasmi ya ndoa yao itafanyika.

Kumekuwa na habari mbalimbali kuhusu ndoa ya Kanye na Kim, huku wengine wakidai kuwa couple hiyo tayari imeshafunga ndoa, habari ambazo Kim Kardashian amezikanusha hivi karibuni kupitia twitter kuwa bado hawajafunga ndoa.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. iyo yote pesa ndo inawaangaisha, mlipanga ufaransa saiv tena italy, yetu macho

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad