Nisha: Naona Aibu Kuangalia Filamu zangu za Komedi

Msanii wa sanaa za vichekesho nchini, Salma Jabu aka Nisha amesema huingia na aibu kutazama filamu zake za komedi kutokana na vituko anavyovifanya.

Nisha anayetamba na filamu kama Pusi na Paku,Tikisa,Gumzo na Zena na Betina amedai anapoangalia filamu zake halafu mtu akamkumbushia hujificha uso wake kwa aibu.

“Ni ngumu kuamini but huo ndio ukweli, hata mimi nikijitazama huwa naona aibu,ndugu zangu hawaamini yule mtoto mpole anayeng’ata kidole hadi ukubwani,Leo kwenye tv anafanya hayo.. Thanx God ujumbe umefika nimeweza kuwafanya watu waamini mimi mcharuko hahaah,” amesema Nisha.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad