Wanaouza na Kuwafanyisha Biashara ya Umalaya Wasichana China Wanaswa

BAADA ya kuwepo malalamiko ya wasichana wadogo wa nchini kusafirishwa kwenda China kutumikishwa katika biashara ya ngono pamoja na dawa za kulevya, sasa serikali imenasa mtandao huo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe alitoa taarifa hiyo juzi bungeni wakati akihitimisha michango kuhusu bajeti yake kwa mwaka wa fedha 2014/15 iliyopitishwa.

Chikawe ambaye hata hivyo hakufafanua kwa undani wa mtandao huo ulivyokamatwa, alieleza Bunge namna watoto hao wanavyopatikana kabla ya kufikishwa nchi hiyo ya nje.

Kwa mujibu wa Waziri, watu hao wamekuwa wakichukua watoto wadogo na kuwaambia kwamba wanawapeleka China hususani mji wa Guanzhou kuwaajiri kwenye saluni na maduka.

Alisema kinara wa usafirishaji amekuwa akitambuliwa kwa jina la ‘Mama’ ambaye baada ya kufika nchini humo, huwanyang’anya watoto hao hati zao za kusafiria. Imebainika zipo hata wakala zinazojihusisha na biashara hiyo haramu ya binadamu.

“Wakifika, Mama anawanyang’anya pasipoti zao. Anawaambia ili kuwarudishia, lazima watimize masharti ya kumpa kati ya dola 8,000 na 10,000 baada ya kutumika katika vitendo vya ngono,” alisema Waziri Chikawe.

Aliendelea kueleza kuwa wanaposhindwa kutimiza masharti hayo, hukutana na Wanigeria ambao huwapa hati bandia za kusafiria na kisha kuwaingiza katika biashara ya kusafirisha dawa za kulevya kwenda nchi mbalimbali.

“Tumenasa mtandao huu…polisi imenasa mtandao,” alisema Waziri na kutoa mfano kwamba hivi karibuni, alikamatwa mtu akiwa na hati ya kusafiria akimpelekea binti mmoja. Alisema binti huyo alipoulizwa juu ya hati hiyo, alikuwa hafahamu anakokwenda.

Awali, taarifa juu ya kuwepo usafirishaji wa wasichana wadogo kwenda China kwa ajili ya kutumikishwa katika ngono, ilitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe baada ya kutoka ziarani nchini humo.

Membe alisema serikali inashirikiana na ubalozi wa China katika kubaini wahusika wa biashara hiyo sanjari na mkakati wa kuhakikisha wasichana hao wanarudishwa nchini.

Akielezea mikakati ya serikali katika kukabili biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu, Waziri Chikawe alisema katika mwaka wa fedha 2013/2014 Sekretarieti ya kupambana na biashara hiyo imeratibu vikao vinne vya Kamati ya kupambana nayo.

Aidha imeandaa kitabu cha anuani na majina ya watoa huduma kwa waathirika wa biashara haramu ya usafirishaji binadamu na vilevile kutengeneza rasimu ya kanuni za sheria ya kupambana na biashara hiyo nchini.

Katika mwaka wa fedha 2014/2015 sekretarieti itakamilisha kutengeneza kanuni za Sheria ya kupambana na biashara hiyo ya mwaka 2008. Pia itatoa elimu na kuimarisha mikakati ya kupambana na biashara hiyo ya kusafirisha binadamu.

Watanzania zaidi ya 100 wakiwemo wasichana 20 wamedaiwa wapo gerezani nchini China wakijihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Post a Comment

5 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kwa kweli serikali ikomeshe hii hali na iwasaidie hao wa dada maana wamelalamika sanaaa.

    ReplyDelete
  2. kama wamelalamika wasaidiwe ipasavyo

    ReplyDelete
  3. mie mwenyewe nimenusurika, kupelekwa nje... Dah sio xri ni mungu tu kaniokoa

    ReplyDelete
  4. so kuwen makin tu dada zangu na watu watakao kurubun kwenda nje et kwa kigezo cha kaz!hawa watu wac2mie chanc ya umackn wet kuwa tajrsha wao!aiseee inauma sana,kwel Mungu anahuruma ndo maana hata mm cjawa mungu,lait nngekuwa mungu hawa wa mama nnge waangamza inaumaaa.

    ReplyDelete
  5. DOLA 10000 ZDSHA NA SH 1650 !DAA!N HELA NYNG SANA NA KWA BIASHARA YENYE RISK KAMA ILE,AF NACKIA ET HELA YAKULA, KUVAA,PANGO UNAJTEGEMEA MWENYEWE DU,

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad