Mke wa Mtu Ajeruhiwa Baada ya Kumfumania Mume Wake Akibinjuka na House Girl

Stori: issa mnally via GPL
UBABE! Tofauti na inavyoaminika na wengi kuwa mfumaniwaji huwa mpole, kibao kimebadilika, mfanyakazi wa ndani aliyejulikana kwa jina la Niachie amegeuka mbogo na kumchoma bisibisi bosi wake, Amina ‘Mama Zai’ aliyemfumania akiwa na mumewe aitwaye Amri.

Tukio hilo lilitokea juzikati maeneo ya Mbagala jijini Dar ambako mama Zai alimwekea mtego mfanyakazi wake huyo wa ndani baada ya kubaini kuwa alikuwa akitembea na mumewe wakati yeye akiwa kazini.

ISHU ILIVYOANZA
Akizungumza na paparazi wa kitengo maalum cha kufichua maovu (OFM) siku mbili kabla ya tukio, mama Zai alidai kuwa mumewe ana kawaida ya kufanya mapenzi na mfanyakazi wao wa ndani wakati yeye akiwa kazini hivyo akaandaa mtego ili kukomesha tabia hiyo.

KUMBE NI NESI
Mama Zai alizidi kumwaga data kuwa, yeye ni nesi katika hospitali moja ya mtu binafsi iliyoko Jangwani jijini Dar hivyo akiwa zamu ya usiku, mumewe hutumia mwanya huo kubanjuka na hausigeli.

“Ananivizia nikitoka tu na akijua nimeshafika mbali, anaingia chumbani kwa hausigeli na kuvunja naye amri ya sita,” alidai mama huyo.

MTEGO WANASA
Mama huyo alisema ili kufanikisha zoezi la kumnasa mumewe, alijifanya anakwenda zamu ya usiku kisha akajifungia stoo ili aweze kufanya fumanizi matata.

Kama kawa, OFM ilitia timu nyumbani kwa mama huyo ikiwa kamili na zana zake, ikakita kambi katika baa moja iliyo jirani na nyumba hiyo na ilipofika saa tano usiku, ishu ikatiki, baba Zai aliingia katika chumba cha mfanyakazi huyo kwa lengo la ‘kuharibu’.

'MISS IN ACTION’
Wakati makamanda wa OFM wakiwa ‘wanaseti’ kamera zao huku wakisubiri polisi na mwenyekiti wa serikali za mtaa wafike eneo hilo, mama Zai alivamia chumba hicho (alihofia baba atamaliza mchezo) na purukushani ya nguvu ikaanza.

Katika harakati za kujinasua katika kipigo cha bosi wake, hausigeli huyo aliokota bisibisi na kumchoma mama mwenye nyumba shingoni kisha kutimua mbio huku mume naye akiingia mitini.

Post a Comment

12 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. eee!kama hamridhishi mmeo lazima atafute wa kuongezea.

    ReplyDelete
    Replies
    1. wewe cjui ni senge?!!! pumbavu!! au wewe janamke jizi?!!!

      Delete
  2. we annoy hapo juu fala nini wanaume wnakuridhishwa

    ReplyDelete
  3. Wewe kwenye uchungu usizidishe uchungu hawa wanaume weshawahi kuridhishwa!!!? Omba Mungu yasitokee kwa upande wako.

    ReplyDelete
  4. Uislamu mwisho wa 4.....mungu alivyosema kama unauwezo oa wake wa wili mpk w4 hakumaanisha kipato ni urijali wako....tuuu.....

    ReplyDelete
  5. anonymous 9.24 & 9.25 huyo hapo juu ni msenge au changudoa ndio maana kaandika huo uharo.

    ReplyDelete
  6. wanaume hawana hakili jamani we acha tuu

    ReplyDelete
  7. Yote ni kumwachia Mungu.Tuzidi kuombeana.

    ReplyDelete
  8. wanaume akili zao zikishahamia chini huwa hawafikirii hata madhara baadaye una familia yako ,watoto jamani hivi huwa mnakumbwa na shetani gani

    ReplyDelete
  9. w,ume wote haramu...

    ReplyDelete
  10. Pepo la ngono lina nguvu......si unaona bwana mpaka watu wanabaka....wanalala na machizi...unakuta dem mjamzito then yuko stendi asubuhi anaomba omba...sema dizaini nesi na yeye ana bwana wa night shift...mana hakufanikiwa zaido kajeruhiwa

    ReplyDelete
  11. km hayajakukuta huwez jua uchungu wake rohon! wanaume ni mashetan,hawana huruma hata aibu! Hata umpe ucku kucha!!! Ukitoka ana lala na hgirl pia! Inaumaaaaaa!!!!!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad