Rekodi mpya iliyoandikwa na Nigeria usiku wa jana kwenye kombe la dunia

Timu ya taifa ya Nigeria ‘Super Eagles’ jana iliweka rekodi mpya katika michuano ya kombe la dunia, baada ya ushindi dhidi ya Bosnia.
Super Eagles jana walipata ushindi wa kwanza kwenye michuano hiyo tangu mashindano ya mwaka 1998 yaliyofanyika Ufaransa.
Goli pekee la mshambuliaji wa Stoke City Peter Odemwingie lilivunja mkosi wa kutokushinda mechi kwa Nigeria katika kipindi cha miaka 16 iliyopita.
Nigeria sasa wamefikisha pointi 4 wakishika nafasi ya pili nyuma ya Argentina ambao tayari wameshafuzu.
Mechi za mwisho ya kundi hilo zitakazowakutanisha Nigeria vs Argentina na Iran vs Bosnia ndio zitaamua timu gani itakayoungana na Argentina kwenda kwenye hatua ya pili ya michuano hiyo

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad