Good News!! Staa wa Bongo Fleva kwenye collabo na Fally Ipupa

Good news ninayotaka kukusogezea ni hii kuhusu msanii wa Bongo Fleva kutokea Tip Top Connection, Tunda Man amesema tayari amefanya mazungumzo na  msanii wa Congo maarufu Fally Ipupa kuhusiana na collabo yao.

Akiongea na millardayo.com alisema; “Fally Ipupa nilipiga naye story akaniambia anataka dola 1000 ambayo ilitakiwa nimkabidhi yeye ili nifanye naye featuring mwaka jana nafikiri ndio nilipiga naye stori hizo, akaniambia basi powa nikipata tu hiyo hela nimkabidhi.

Mwezi wa kumi na mbili Babu Tale alimtumia ngoma na alisema haiwezi kuzidi January atakuwa ameshaituma sauti  kwa hiyo anasikiliza kwanza ngoma akishaipitisha atatuambia sisi tumtumia mpunga, nafikiri sauti yake itakuwa tayari kwa hiyo alisema yuko Ufaransa anahitaji ile Beat kwa sababu yeye ngoma zake nyingi uwa anafanyia kule na Beat yetu sisi tulikuwa tumeipiga kwa kutumia computer kwa hiyo ilitubidi tuwachukue wakina kibosho wapige drums, tumewachukua Musa Mipango wapige bass ile ki-live live watu, bendi wamehusika ili yeye mwenyewe aweze kuimba kwa hiyo mimi na management yangu tuko sawa tumemtumia Beat kama akiipitisha basi tutamtumia hela yake dola 1000″– Tunda Man
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad