Jina Kabula na Mwanamuziki Bushoke Wapigana Kibuti, Kabula Atoa ya Rohoni

MSANII wa filamu Bongo , Miriam Jolwa ‘ Jini Kabula ’
na aliyekuwa mpenzi wake wa muda mrefu , Ruta
Maximilian Bushoke wamemwagana na hakuna cha
ndoa tena .

Akizungumza Kabula alitoa ya rohoni na
kusema kuwa wamefikia hatua hiyo baada ya kuona
mwenzake haoneshi msimamo katika mkakati wao wa
kuoana hivyo kwa sasa wamebaki kuwa marafiki wa
kawaida tu kwa sababu wote ni wasanii.
“Tumeshaachana , mwaka huu nimeuanza kwa kuwa
bize na mambo yangu mengine ya kikazi siyo mapenzi
tena . Tulikuwa tumepanga vizuri kwamba tutaoana na
kuamini hivyo kwa kipindi chote alichokuwa nchini
Afrika Kusini. ”
“Baada ya mwenzangu kutua Bongo , hakuonesha dalili
yoyote ya kutekeleza hilo suala la ndoa . Sikuwa na
uwezo wa kusema nimfunge kamba ndiyo nimlazimishe
kumpeleka kwetu tuoane , nimeona bora niachane naye
kwani nimeshachoka na maisha ya uzinifu nahitaji
kuingia katika ndoa , ” alisema Kabula .
Bushoke alipotafutwa kwenye simu hakupatikana lakini
kwa mujibu wa marafiki zake wa karibu wanasema
kuwa amesharudi Afrika Kusini.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad