Wema Sepetu Ajutia Mimba ya Kanumba

Mrembo na mwigizaji wa filamu, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ anadaiwa kujutia mimba yake aliyopachikwa na aliyekuwa staa mkubwa wa sinema za Kibongo, marehemu Steven Kanumba ‘The Great’ wakati wa mapenzi yao.

Chanzo makini kilicho karibu na Wema kilieleza kwamba, mwanadada huyo kwa sasa yupo kwenye wakati mgumu huku akijutia mimba aliyopewa na Kanumba ambayo ilichoropoka kwa bahati mbaya na huyo ndiye mwanaume pekee aliyewahi kumpa ujauzito.

“Yaani Wema anajutia kweli kwamba kwa nini hakuzaa na Kanumba kwani ndiye mwanaume pekee aliyewahi kumpa ujauzito ambapo kwa sasa anatafuta mtoto lakini hapati, yaani yupo kwenye wakati mgumu sana akikuelezea mwenyewe unaweza kulia kwani ana simulizi ya kusikitisha kuhusu maisha yake na Kanumba.
“Hii yote inatokana na kwamba kwa sasa anatamani kuitwa mama lakini hapati hivyo kujikuta akiukumbuka ule ujauzito wa Kanumba anateseka kweli moyoni,” kilisema chanzo hicho.

Alipoulizwa Wema kuhusu ishu hiyo alikiri na kuonesha namna gani anateseka moyoni.
“Nateseka kweli, tangu ilipotokea kwa Kanumba haijawahi kutokea tena. Hakuna mtu ambaye hapendi kuwa mama, nazidi kumuomba Mungu huenda na mimi itatokea nitapata,” alisema Wema.

GPL

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kama Wema hakutoa hiyo mimba kwa nini ajute sasa. Mimba iliyotoka kwa bahati mbaya haiwezi kumfanya mtu ajute na kukumbuka. Hiyo ni dalili ya maoksa ya nyuma aliyofanya.

    Unaweza kuchagua nini cha kufanya lakini huwezi kuchagua matokeo.

    ReplyDelete
  2. Hakna cha mimba kutoka,HAZAI uyo mdada!!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad