Dude Asema Akili Yake ni Mbovu Ndiomana Anashindwa Kuoa

Mwigizaji nguli wa filamu za hapa Bongo, Kulwa Kikumba, amesema licha ya kuishi na mzazi mwenzie kwa zaidi ya miaka kumi, anashindwa kuoa kwa sababu akili yake siyo nzuri.



Akipiga stori mbili tatu na mwanahabari wa GPL, Dude alisema linapokuja suala la kulaumiwa kuchelewa kuoa, anastahili kwani hakuna kitu kinachomsababisha asioe zaidi ya akili yake kuwa mbovu.

“Mimi akili yangu tu bwana ndiyo mbovu, hakuna kitu cha ziada ninachoweza kujitetea, kama kuona ningeoa siku nyingi sana, nashindwa basi tu,” alisema Dude.

GPL

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad