Flora Mvungi: Bongo Movie Hatuna Ushirikiano Hata Kidogo

Mwigizaji wa filamu  ambae ameingia kwenye bongo fleva, Flora Mvungi ‘H.Mama’ amefunguka na kusema kuwa wasanii wengi wa bongo movie hawapendani ndiomaana wanashindwa kufika mbali kisanaa.

Akinukuliwa na Gazeti moja la burudani, Flora alisema “Tukitaka kufanikiwa lazima sote letu liwe moja ili tufanye kitu kizuri,siku zote umoja ni nguvu cha msingi tukiamua kufanya kazi tusiangalie huyu bado msanii chipukizi siwezi kufanya naye kazi wote tushirikiane ili tufanye vitu bora na kupige hatua”.

Aliendelea kusema kuwa wasanii ambao tayari wamesha kuwa mastaa wakitafutwa ili afanye naye kazi lazima atataka malipo makubwa na ukiangalia bado chipukizi basi ndio mwanzo wa kakata tamaa.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Sitdhani kama wasanii wana roho mbaya, ila wewe dada unatakiwa ujiheshimu na mavazi yako ili uweze ku endana na wasanii wenzako. Jaribu sana kijieshimu na sio kuonyesha mapaja yako yaliosinyaa

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad