Nimemtongoza Jana, Leo Anataka Nimtumie Hela

Kuna msichana niliwahi kuonana nae mara1 ni rafiki wa dadaangu, tulionana nilipoenda kumtembelea sista nikahisi kumpenda, jumapili kulikuwa na event ya kifamilia nikaonana naye, safari hii nikawa siriaz kumbana nimsomeshe hadi kieleweke.

Bahati nzuri tulipotoka kwenye event tulisafiri pamoja nikakaa naye kwenye siti zinazofatana, nilimtongoza though hakunipa jibu la moja kwa moja kunikubalia but alikuwa anaonyesha kuelekea kukubali, nilimwomba namba yake akanipa. Kesho yake ambayo ni jana akanichokoza kupitia msg, akanisalimia nami nikarespond.

Si nikahisi mtoto kashakolea, ile nataka nianze kumchokoza anipe jibu langu mara akatuma meseji 'Nasikia njaa', duh ile kuendelea kuchat nikagundua anamaanisha nimtumie hela. Eti ndugu wananchi, huyu ni wife material kweli au najiingiza kwenye majanga? Maana mtu mwenyewe hela za kuokoteza.
Tags

Post a Comment

4 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. majanga hayo achana nae!!

    ReplyDelete
  2. Mbona hilo ni jambo la kawaida ,sasa kama akufiche nini kama kweli anaumwa?acha kukwepa majukumu wewe.ukiwa mbahili utawasikia tu hao viumbe.halafu unaanzaje kutafuta wife wakati huna mbele wala nyuma? Jipange baba usifikiri kumiliki wife ni lelemama,wanamahitaji hao na ni wajibu wako kuyatimiza.

    ReplyDelete
  3. Usishangae kaka siku hizi hapendwi mtu bali pesa zake ndio maana mwana dada kaanza kutafuta pesa ndicho anachotaka kwako

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hakuna mwanamke ambay siku hizi hapendi petha tena huyo kakuanzia pazuri kuna mshkaji wangu ndo siku ya kwanza kumeet na mchuchu wake hafu dem anaishi Kigamboni na jamaa yupo Mpiji Magoe huko Mbezi mwisho ndani ndani kabisa

      Demu alimwambia hapandi daladala anachukua tax hafu akija mshkaji amlipe dreva jamaa alisanda hafu hana kazi ya maana ni zile za kudunduliza hafu matatizo kwake hadi uvunguni......

      Delete

Top Post Ad

Below Post Ad