Al Shabaab Wavamia Tena Kenya, Watoa Onyo Kali Kwa Wananchi

Mamlaka nchini Kenya imesema kuwa walinda usalama wamekabiliana na washukiwa wa kundi la wapiganaji wa kiislamu la Al- Shaabab, katika wilaya ya Ijara katika kaunti ya Garissa Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.

Mapema, wapiganaji hao waliokisiwa kuwa zaidi ya 50 kutoka Somalia, wanasemekana kushambulia kambi za polisi katika eneo la Yumbis, takriban kilomita 30 kutoka Daadab.

Wavamizi wa Al-Shabaab waliteka vijiji vitatu na kupeperusha bendera yao Kaskazini Mashariki mwa Kenya kwa muda kabla ya maafisa wa polisi nchini kenya kuwasili na kuwatimua. Vijiji vilivyovamiwa ni Ramu iliyoko Mandera, na vijiji vya Yumbis na Holugho vilivyoko Garissa.

Walioshuhudia wamesema kuwa wapiganaji hao waliikejeli serikali ya Kenya na wakawaonya wanavijiji kwa kuendelea kushirikiana na serikali ya Kenya.

Japo viongozi nchini Kenya wamesema kuwa maafisa wa usalama wamewafukuza  wanavijiji wenyeji wa Yombis wanaodai kuwa bado wapiganaji hao wako
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad