Batuli Achezea Sharubu za Kajala Masanja......

Imelda Mtema
STAA wa filamu za Kibongo, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’ ameonekana kuchezea ‘sharubu’ za Kajala baada kuweka picha ya kiazi kwenye mtandao wake wa kijamii wa Instagram kitu ambacho kimeonekana ni kumkejeli staa mwenzake huyo kutokana na Wema Sepetu kumuita kiazi.


Akichezesha taya na Amani baada ya kubanwa kwa nini aliweka picha hiyo kwenye Instagram yake, alisema kuwa yeye ana maamuzi ya kuweka kitu chochote kwenye ukurasa wake huo hivyo kama kuna mtu anajishtukia shauri yake.

Kwa upande wa Kajala alipoulizwa kama kuna tatizo lolote kati yake na Batuli alifunguka;
“Sijui kama mtu ana bifu na mimi basi ni yeye tu na kama mtu anaposti kitu kwa  ajili ya kuniumiza naona ni kazi bure tu kwa kuwa vitu hivyo vinapita na maisha yanaendelea siku zote.”
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. kazi kweeeeeeeeeeeeeeliiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad