Breaking News:Ule Mkataba Wenye Utata Kati ya Mchezaji Ramadhani Singano na Team ya Simba Wavunjwa na TFF

LEO sakata la kiungo mshambuliaji wa Simba, Ramadhan Singano 'Messi' lilikuwa linasikilizwa kwenye ofisi za TFF ambapo pandehizo  mbili zilikutana chini ya TFF.

Baada ya kikao kirefu muafaka uliofikiwa chini ya TFF  kuvunjwa kwa mikataba yote miwili ambayo inatofautiana.

Kikao kimeamua mkataba alionao Messi uvunjwe na mkataba walionao Simba uvunjwe waingie makubaliano mapya.

Upande wa Singano haujakubaliana na maamuzi hayo kwa sababu unamtaka akubaliane na Simba tena. Lakini kwa mujibu wake ni kwamba anatakiwa kuwa huru kama mkataba umevunjwa na sio kukubaliana upya na Simba. Singano anataka kuwa mchezaji huru ndipo aamue mwenyewe kama kuongea na Simba au klabu nyingine.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad