Christian Bella: Hakuna Msanii Asiyependa Kufika Alipofika Diamond Platnumz

Mwanamuziki Christian Bella
Christian Bella anaamini kuwa kikwazo cha wasanii wengi kukua kutokuwa na management. Bella ameiambia Bongo5 kuwa kila msanii ana lengo la kwenda mbali zaidi lakini tatizo lipo kwenye management.
“Muziki wetu bado una matatizo mengi ndo maana unaona kuna wakati unahitaji kufanya kitu lakini unashindwa. Hakuna msanii asiyependa kufika alipofika Diamond, kila mtu anataka, tatizo ni management,” amesema msanii huyo.

“Kila msanii huwezi kutumia pesa yako ya mfukoni kutengeneza video, hautaweza kufika popote. Management ndIo inaweza kukusimaMia kila kitu, lakini sisi hapa kila kitu anafanya msanii huyo huyo, hatuwezi.”

Chanzo: Bongo5

Tanzania Hottest Celebrity Gossip News

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad