Licha ya Kujifungua Hivi Karibu Aunty Ezekiel Uzuri wake Pale Pale..Chuma za Reli

KIWANGO! Tofauti na watu wengine ambao maumbile yao hubadilika mara baada ya kujifungua, kwa staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel hali imekuwa tofauti, uzuri na umbo lake limebaki vilevile.

Akizungumza na wahariri sambamba na waandishi wa Global Publishers nyumbani kwake Mwananyamala jijini Dar, Aunt alisema kilichomfanya asinenepe kupita kiasi na kuharibika mwili ni mazoezi sambamba na kufuata ushauri wa vyakula anaopewa hivyo mwili wake kubaki vilevile.


  • “Nachukia ubonge nyanya, namshukuru Mungu pia kwani wengi wakijifungua huwa wananenepa hovyo lakini kwangu mambo yamekuwa tofauti. Niko vilevile, nafikiri pia ni kutokana na kufuata ushauri mzuri wa kula chakula niliopewa,” alisema Aunt.



Mbali na kutobadilika, Aunt alisema kwa sasa muda mwingi anautumia kuwa nyumbani na ubavu wake, Moze Iyobo wakimlea mtoto wao tofauti na zamani alipokuwa na misele ya usiku katika viwanja tofauti vya starehe.
GPL

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. BADO HATA 40 BADO UNAVUJA DAMU YA UZAZI ARAFU UNAPICHA MAPICHA YA NUSU UCHI SHAM ON U. TULIA UPONE NDOMAANA ZIWEKWA SIKU 40 SIO 20 PAKATA MTOTO AKUE KWA JOTO LAKO MAMIII

    ReplyDelete
  2. UNACHEKESHA UBONGE WA SIKU ISHILINI AU MWEZI , SUBIRI MAMA

    ReplyDelete
  3. Kusema ukweli sijui nisemaje enyi mnaoandika hoja zenu lakini kwa kiswahili kibovu ile mbaya shuleni mlikuwa hamko makini na somo la kiswahili au ndivyo mlivyofundishwa na waalimu wenu kuandika kiswahili kibovu?Kweli bongo elimu sasa ni ya kubahatisha taifa la kesho au keshokutwa namna hiyo duh!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad