Mwanamuziki ALI KIBA Adaiwa Kuiba Maudhui ya Wimbo wa Chekecha Kwa Msanii Chipukizi

ALI KIBA
Msanii chipukizi wa muziki wa kizazi kipya Bongo kutoka Mbeya aliyefahamika kwa jina la Ahmad A.K.A AD amelalamikia kuibiwa kwa maudhui ya wimbo wa Chekecha na Ally Kiba.

Akifunguka jana kupitia kipindi cha “The Jump off” cha Times fm, AD anadai alikutana na Ally kwenye show Mbeya akimtaka wafanye “collabo”, AD alidai alimpa vionjo Ally lakini baada ya miezi kadhaa akashangazwa kuisikia chekecha redioni.


  • “Tulikutana Mbeya nikamwambia bro nina Idea kali, sijamtafuta bado ila next week nakuja dar nitamtafuta then taratibu zingine zitafuata” alisema Ahmad


Katika hatua nyingine “The jump off”, ilimtafuta meneja wa kundi linalowajumuisha Ally Kiba na Abdu Kiba( kiba square) Kapasta 4 real, ambaye amedai kwamba huo ni uzushi na jamaa ana lengo la kutafuta umaarufu kupitia mgongo wa Ally Kiba.


  • “Ile nyimbo Ally kaandika studio, melody pamoja na kila kitu so huyo jamaa aache ujinga wake,asizingue tutampeleka kwenye viombo vya sharia asichezee kazi za watu” alimaliza Kapasta.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad