Sauti Sol waonesha mfano kwa kum-support Diamond kwenye tuzo za MTV MAMA 2015

Kundi la Sauti Sol kutoka Kenya ambalo linaiwakilisha Afrika Mashariki kwenye BET Awards 2015 zinazotarajiwa kutolewa Jumapili hii June 28 nchini Marekani, wameonesha mfano unaopaswa kuigwa na wasanii pamoja na mashabiki wa muziki wa Tanzania kuwaunga mkono wasanii wetu wanaowania tuzo za kimataifa.

Kupitia akaunti yao ya Instagram Sauti Sol wameutambua uwakilishi wa Diamond katika tuzo za BET za mwaka jana, na kumpigia kampeni ya kupigiwa kura kwenye tuzo za MTV MAMA 2015 ambapo anawania tuzo tatu.

“Mwaka jana ni @diamondplatnumz ndiye aliyetuwakilisha nchini Marekani kwenye #BETAwards2014 This year we’re so humbled to be the ones representing African music at @bet_intl @bet_africa #Betawards2015 on 28th June at the Nokia Theatre, LA. Shukran sana kwa sapoti aliyetuonyesha. Je, wamkubali? Haiya basi, check link kwenye bio ya @wcb_wasafi kisha umpigie kura #BestMale As many times as you possibly can, ni wakati wa Afrika mashariki”

Endelea kuwapigia kura Diamond na Vanessa wanaoiwakilisha Tanzania kwenye tuzo za MTV MAMA mwaka huu. Diamond anashindania vipengele vitatu, Best Male, Best Collaboration na Best Live. Vee Money anawania kipengele kimoja cha Best Female.

Ingia hapa uweze kuwapigia kura mara nyingi uwezevyo.

Watanzania tuungane kuwapigia kura wasanii wote wanaotajwa kuwania tuzo za kimataifa ili kusaidia kuukuza muziki wa nyumbani.
Tags

Post a Comment

4 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. big up diamond tupo pamoja kwa saana tu

    ReplyDelete
  2. Inasikitisha sana kusikia haya tunayosikia ya vita ama uadui kwa KIJANA DIAMOND kwa anavyojituma kisha kiwepesi tena BILA HAYA mtu unaamua tu kumchukia kiasi cha kufikia hatua kuwavunja moyo hata wale wanaomsupport! LKN TIME WILL TELL. Lets wait and see. Muogopeni Mungu jamani.

    ReplyDelete
  3. binadam hatengui alipangalo mungu ilamungu hutengua alipangalo mja/binadam... we support u bro diamond............

    ReplyDelete
  4. Mtu kuwa na maendeleo ni sumu kubwa kwa asilimia kubwa ya Wa TZ,mtu anayejituma na kupata maendeleo kwao ni shiiiiiiida,zitaanza fitna na majungu almradi huyo mtu aonekane na kasoro lakini ukiangalia chanzo cha chuki ni maendeleo tu ya huyo anayechukiwa,watz acheni hizo thaminini vya kwenu utumwa wa vyawatu mpaka lini?

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad