Steve Nyerere Awapa Makavu Baadhi ya Mastaa Wenzake wa Bongo Movies

Staa wa bongo movies, Steve Mengere ‘ Steve Nyerere’ amesema hana mpango na shutuma mbalimbali zinazosemwa  na baadhi ya  wasanii wenzake kwani Mungu atamlipa kutokana  na uvumilivu wake

Steve nyerere aliyasema hayo na kuweka wazi kuwa kuna watu wanamchafua ambao hawana ishu yoyote hapa mjini zaidi ya kutupia picha kwenye mitao ya kijamii na kujinadi kwa nyumba nzuri na na magari ya kuazima.

“ Unajua kuna mambo kibao ya kufanya katika jamii lakini watu hawayaoni zaidi ya majungu  tu  hao watu hawana la kufanya katika maisha yao wao ni kuwaza tu sherehe itafanyika lini ili wafike mapema  na kuwafunika hata  wanakamati “alisema Steve Nyerere.

Alizidi kuhoji Steve Nyerere kuwa kila kukicha  anazidi kuchafuliwa bila kuelewa ni nini kinaendelea na kama kuna tatizo kubwa aulizwe kuliko kusimangwa  bila mpango.

Mungu atanilipia kwa kweli  kwa yote wanaonnipangia hayatanifika ila nataka kusema  hivi majunguhayana maana yoyote kusingiziana mamba ambayo hayana maana na kuchafuliana  majina bila ya mpangilio” aliongeza Steve.

Kama hiyo haitoshi  Steve Nyerere alidai katika mipangilio yote  ambayo anashutumiwa yeye anatafutwa na kupewa kazi kwa maana hiyo anaaminikana ndio maana anapata nafasi kama hizo.

KIU

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad