Wawania Urais Waukacha Mdahalo...Pole Mafuruki, Hiyo Ndiyo CCM Bana

Si jambo geni lililotokea leo. Si jambo la kustaajabisha wagombea watarajiwa wa CCM kukimbia midahalo. Mafuruki pole,hujaijua CCM. CCM haina watu wenye hoja za haja za moja kwa moja-live arguments. CCM haina wajibu maswali ya moja kwa moja-live response.

CCM imejaa watumia fedha kushinda uchaguzini. Kuwaweka kwenye mdahalo wanachama wa CCM ni kutaka kuwadhalilisha na kuwaaibisha. Ni kutaka kuwavua nguo mbele ya halaiki. Pole Mafuruki. CCM is not reachable,try again later.

Labda kungekuwa na vyombo vya dola pembeni,wanaCCM wangetoa pointi. Wangetema cheche. Kiufupi,sisi ni waeupe na watupu kwenye midahalo. Hata Katibu Mkuu wa zamani wa CCM,Yusuf Makamba aliona hilo. Akapiga marufuku kushiriki midahalo. Mafuruki ulikuwa hujui? Pole.

CCM inabebwa na ujinga na umaskini wa watanzania. Ushindi kwanza,hoja baadaye.Aibu kukimbia,heshima imelindwa lakini. Hiyo ndiyo CCM!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad