AJALI Mbaya ya Basi Mkoani Dodoma, Abiria zaidi ya 20 Wamefariki Dunia na 38 Wamejeruhiwa...

Taarifa kutoka mkoani Dodoma zinasema zaidi. Abiria zaidi ya 20 wamefariki dunia usiku huu, huku zaidi ya abiria 38 wakijeruhiwa vibaya baada ya basi la kampuni ya SIMIYU EXPRESS walilokua wakisafiria kutoka Mwanza kwenda DSM kupasuka tairi na kuacha njia na kugonga mbuyu na kisha kupinduka.

Taarifa zinasema ajali hiyo ni mbaya sana kuwahi kutokea mkoani Dodoma, hadi hivi sasa bado kuna miili haijatolewa kwenye mabaki ya basi hilo kutokana na kuharibika vibaya na kubaki mithili ya nyama.
MWENYEZI MUNGU AZILAZE MAHALA PEMA PEPONI ROHO ZA MAREHEMU NA KUWAPA NGUVU FAMILIA ZOTE ZA MAREHEMU AMEEN

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Tanzania inaongoza kwa ajali za barabarani nahisi uzembe wa madreva na wana usalama balabalani vimechangia

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad