Utendaji wa Magufuli na Mfano wa Msichana wa Kazi za Ndani...

Kuna wanaume wengi sana walio wahi kuoa wasichana wao wa kazi (house girl) sio kwamba wanaume hao wanaamua kuwaoa wafanyakazi wao wa ndani bila sababu, sababu kubwa kabisa huwa ni kuvutiwa kwa uchapa kazi wao, utiifu nidham na heshima ambazo huonyesha mbele ya mabosi wao.

Unakuta mfanyakazi huyo wa ndani anafanya mambo Makubwa hata kumzidi mke ambae hajui watoto wamekula au hawajala, wanaumwa ama la.

Kwa vile wanaume wengi huvutiwa na tabia hizi za kujituma wakati mwingine hupelekea mwanaume kuanza mahusiano ya kimapenzi na mfanyakazi wake ambae humjali kwa kila kitu hapo nyumbani, mapenzi yakikolea mwanaume wakati mwingine huchukua maamuzi ya kufunga ndoa na mfanyakazi wake.

Lakini bahati mbaya kabisa mwanamke huyu baada ya kuolewa huanza kuziacha zile tabia ambazo ndo zilizomvutia mwanaume mpaka akafikia maamuzi ya kumuoa, majuto makubwa hufuata kwa mwanaume kwakuwa huwa hana uwezo tena wa kuachana nae.

Ninavyo fikiri mimi, kila kiongozi wa ngazi ya juu huwa tunamchagua kwa kuvutiwa na sera zake lakini baada ya muda mfupi huwa tunajuta na kuanza kujilaumu kwa uchaguzi wetu.

Swali, je? Tukimpa nchi Magufuli ataendelea na uchapa kazi wake au atabweteka baada ya kuwa rais?

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. duu! hilo nalo nene coz rais sio mtendaji mkuu wa serikali kuna wabunge na mawaziri akiwalea na kuwalinda hatokuwa na tofauti na kikwete

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad