Hatimae Polisi Kutoa Tamko CCM Kuzidisha Muda wa Kampeni Baada ya NEC Kudai ilikuwa Kazi yao Kuwazuia CCM


Kamishna wa operesheni mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini Paul Chagonja
Jeshi la Polisi nchini Tanzania limesema kuwa litatoa tamko la jeshi hilo juu ya Chama cha Mapinduzi kuzidisha muda wakati wa Uzinduzi wa Kampeni za chama hicho wiki iliyopita.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mdahalo wa wadau wa uchaguzi leo jijini Dar es salaam Kamishna wa Mafunzo na Operasheni wa Jeshi la Polisi CP Paul Chagonja amesema kuwa wanashughulikia suala hilo na muda ukifika watatoa tamko.
Ameongeza kuwa ili uchaguzi uwe wa Amani ni lazima watu wote watimize wajibu wao.
Kwa upande wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi iliwakilishwa na Jaji Mstaafu John Mkwawa amevitaka vyama vya siasa kuzingatia maadili ya uchaguzi waliosaini ili kulinda amani na kuepusha migogoro na uvunjifu wa Amani.
Kwa upande wa mwakilishi toka chama cha ADC Mwanaisha Yemba amevitaka vyama vyenye vikundi vya ulinzi kuwapa sare na alama maalum walinzi wao ili watambuliwe na kila mtu ili wakifanya vujo iwe rahisi kutambulika.

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. MAKAO MAKUU YA POLISI CHONDE CHONDE ACHENI HIZO.WEWE KAGONJA MTUMWA USIE NA AIBU WA KIKWETE UTOE TAMKO LA KUMPINGA KIKWETE USITUONE SISI KUWA NI MAZUZU ZUZU NI WEWE NA ANGALI DOLA YA KIKWETE INAISHIA OCTOBA 25 JIANDAE KWA MKONO MREFU WA SHERIA.KWA TAARIFA UAMUZI WA KUMCHAGUA LOWASSA TUMEKWISHA UFANYA YEYE KWA SASA ATAKUA ANAPUNGA MKONO TUU HAONGEI MTAMZULIA NENO MUNGU YUPO PAMOJA NA SISI MALOFA

    ReplyDelete
  2. This is non-sense. Mnashondwa kutoa tamko lolote kwa sababu nitahutubia ccm. Iko siku, na sisi mbali sana, ni 25/10/2015 watanzania watakapochukua Kalam na kuamua IMETOSHA, CCM BASI TENA

    ReplyDelete
  3. KAGONJA WAKALA WA KIKWETE UTOE MSIMAMO WA POLISI KUHUSU CCM KUZIDISHA MUDA WA KAMPENI.HUU NI UJINGA MKUBWA WA KAGONJA UNAONAJE UKAKAA KIMYA USUBIRI KIPIGO OCTOBA 25.TENA ANGALIA KAGONJA JINA LAKO TAYARI TUMEKWISHA LIORODHESHA KWA MASHTAKA YA UHALIFU WA KUTUMIA BUNDUKI KUWADHURU RAIA WASIO NA SILAHA WALA HATIA KUWASABABISHIA ULEMAVU WA MAISHA.JIANDAE KWA MASHTAKA YA MSINGI ISHIRINI NA NANE.UTASWEKWA RUMANDE SEGEREA DHAMANA ITAZUIWA NA HUKO SEGEREA UTAPATA MAPOKEZI YA HESHIMA KWA WABABE JELA KISHA KISHA.JELA INAKUSUBIRI

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad