Huu Ndio Mpango wa Ex wa Zari na Mpambe Wake wa Kutaka Kuharibu Furaha ya Ujio wa Tiffah Kwa Diamond na Zari

Ulimwengu una maajabu mengi na mitandao ya kijamii inatusaidia kuyafahamu. Uhusiano wa Diamond na Zari the Bosslady haujawahi kupokelewa vizuri na ex wake Ivan aliyezaa naye watoto watatu wa kiume.

Watoto hao wameendelea kuwa karibu na wazazi wote wawili. Uhusiano wa ulipoanza tu, Ivan kupitia mpambe na rafiki yake wa karibu, King Lawrenc walianzisha vita kwenye mitandao ya kijamii kuwashambulia Diamond na Zari. Hakuna shaka kuwa Ivan amekuwa akionesha hisia zake za kutoupenda uhusiano wao kupitia Lawrenc ambaye amekuwa akiwashambulia mfululizo.

Katika kipindi ambacho tension kati ya Diamond na Alikiba zimefika kileleni hususan kipindi cha kuelekea tuzo za KTMA 2015, Ivan mwenyewe pia alishiriki katika kampeni za kumuombea kura Alikiba. Ni wazi kuwa Ivan bado hajakubali yaishe, na kumuona mke wake wa zamani akiwa na furaha na Diamond ni kitu kinachomkera zaidi.

Na sasa wakati uhusiano wa Diamond na Zari upo katika kilele cha furaha baada ya kujaaliwa mtoto wa kike, Latiffah, kambi ya Ivan kupitia mpambe wake Lawrenc imedhamiria kuitilia doa furaha hiyo.

King Lawrenc ameanza kutupa mashambulizi kwa Diamond na kueleza kile anachoamini kuwa Tiffah ni mtoto wa Ivan! Kwa historia ya kile Lawrenc amekuwa akikisema tangu mastaa hao waanzishe uhusiano, ni wachache wanaoweza kuamini ‘upuuzi’ huu lakini kiukweli hiki ni kitu kinachoweza kuwakosesha raha Diamond na Zari, kama wakiamua kumjali.

Lawrenc alianza kupost picha ya mtoto mchanga na picha ya Ivan na kuandika, “No DNA Needed. The best revenge has shown itself after 9months. Anamaanisha kuwa mtoto huyo ni Tiffah na kwamba Ivan ndio baba yake.

Hadi sasa hakuna picha iliyotolewa inayoonesha sura halisi ya Tiffah hivyo ni ujinga kuamini kuwa aliyoweka Lawrenc ni yake. Na katika yote yanayoondolea, Zari na Diamond hawawezi kuruhusu picha ya mtoto wao ifike kwenye mikono ya adui yao labda kama wao wenyewe wakiamua kuipost kwenye mitandao ya kijamii, kitu ambacho bado hawajakifanya hadi sasa.

Na pengine mambo kama haya ndio yanamfanya mama mzazi asite kuionesha sura ya binti yake huyo. “I swear I wanted to show you her face but she turned away saying, nope i want no drama. She knows y’all can be dramatic. She’d rather stay safe for now… too many judges, advisors, teachers you name it you’ll find it on IG. I bet she can’t deal,” aliandika Zari.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad