Kwanini Wanaume Wengi Walioko Kwenye Ndoa Hufa Mapema na Kuwaacha Wake zao ?

(Kwanini wajane ni wengi kuliko wagane??)
1. Umri mdogo wa kikomo cha maisha “life expectancy” – Kama unafahamu hili jambo linaloitwa “life expectancy” utakubaliana na mimi kwamba umri wa mwanaume wa kuishi ni mdogo sana ukilinganisha na mke wake, hususani kusini mwa jangwa la sahara. Kwa hiyo wanawake wanapewa nafasi kubwa ya kuishi muda mrefu kuliko waume zao.

2. Ugumu katika kufunguka – Utakubaliana na mimi kwamba wanaume ni wagumu sana ten asana kufunguka na kushirikisha mambo yao, wao wako tayari wafe na tai shingoni wakijifanya hawaumii au hawasikii shida. Mkiwa na ishu kwenye ndo mkaitwa sehemu muyaongee yeye kamwe hamumpati, anakwambia mambo yetu tutasuluhisha wenyewe wakati ndani yanamla na kummaliza. Na kwa mtaji huu watakufa sana tu

3. Ugumu katika kusamehe – Kusamehe sio tu kwa faida ya anayesamehewa bali pia kwa afya yaw ewe unayesamehe. Mzigo unaotokana na kusamehe hutuumiza sana mioyo yetu, hata kama mara nyingine tunajifanya hatuna shida yeyote. Unaposamehe unaachilia mzigo mkubwa, wanaume wao ni wagumu sna kusamehe. Wako tayari wakubebe moyoni miaka, na tena watakukumbusha uchungu wao kila wanapokuona. Hii inawala sana bila wao kujua.

4. Tabia hatarishi – Wanaume wengi kwenye ndoa ndio wanaoongoza kushiriki tabia hatarishi kama vile ulevi, anasa, ngono holela na hii huwaweka karibu zaidi na jeneza kuliko wake zao waliowaacha nyumbani wakiwadanganya kuwa wako mkutanoni mkoani.

5. Ugumu katika kujali afya – Ni rahisi sana mwanaume akajisikia vibaya lakini asiende hospitalini kuangalia afya, hata pale anapohimizwa kwenda bado anaweza kukwepa au kubisha au hata kusema kuwa ameshakwenda au ameshakunywa dawa kumbe mwongo. Wako pia ambao wanaweza kupewa dawa na wasizitumie.

6. Msongo wa mawazo – Wanaume ndio wabebaji wakubwa wa shehena za msongo wa mawazo “stress” ingawa kwa nje wanajitahisi sana kuonyesha kuwa mambo yako shwari wakati wanatafunwa ndani. Kaulize hospitalini, wanaokufa kwa presha ya kupanda au ya kushuka, stroke, kusimama kwa moyo, kupasuka kwa mishipa ya damu, matatizo ya mifupa, au kuumwa sana kichwa, halafu uliza ni jinsia gani.

Maisha sio mabaya kiasi hicho, maisha ni mazuri. Chagua kuishi – Chris Mauki

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. wanaume wanatumia miili yao vibaya hasa akiwa na pesa mara yuko na j, y, m, n.k. sasa akizeeka miaka labda 60 anakua yuko hoi kiafya na mara nyingi huwa wanapata stress baada ya kustaafu, hicho ndio kinapelekea wao kufa mapema. Inabidi wajirekebishe hizo tabia zao mbaya! Kama mi muongo angalia wanaume wanaompendeza Mungu wanaishi muda mrefu sana kama kawaida.

    ReplyDelete
  2. Kweli nimekubaliana na hayo pia wanaume wanawahi kufa kwasababu maisha yao yamejaa na changamoto za utafutaji wa maisha kila jambo lazima alipange yeye na awe mfuatiliaji so majukumu mengi ndo yanawatesa

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad