NORA Ananga Wasanii Wanaotumika Kisiasa! Adai Hawaitambui Thamani yao...Kila Mwaka Wanatumika na Kuachwa Solemba

Nora wa Bongo Movies
Msanii wa ‘long time’ kwenye ulimwengu wa filamu, Nuru Nassoro ‘Nora’ amewananga wasanii ambao wanakubali kutumika kisiasa katika kipindi hiki bila kujua madhara watakayopata baada ya uchaguzi.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Nora alisema kuwa, anawashangaa baadhi ya wasanii kukubali kununulika wakati wakijua kuwa, baada ya uchaguzi watamwagwa.
“Jamani mimi nashangaa kuona wasanii tunatumika kwa kiasi hiki, thamani yetu hatuitambui kabisa, kila baada ya miaka mitano tunatumika kisha tunaachwa solemba, yaani dah!” alisema Nora.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Wewe ni mtoto mzuri sana, maana ni mulewa God Bless you....

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad