Baada ya kununua Prado, Nay wa Mitego asema ‘kinachofuata ni Range Rover’

Nay wa Mitego amesema akimaliza ujenzi wa nyumba yake mpya ya kifahari iliyopo Tabata jijini Dar es Salaam, atanunua gari aina ya Range Rover.

Nay ambaye amenunua gari mpya, Prado Land Cruiser hivi karibuni, ameiambia Bongo5 kuwa lengo lake ni kumiliki Range.

“Bado sijapata gari ninayoihitaji, mpango wangu ni Range nikimaliza nyumba yangu ya Tabata,” alisema Nay.

“Hii Prado ni mpya lakini ina kazi maalum. Hii ni kwaajili shows za mikoani. Nimenunua milioni 60, ni mpya kabisa ndio maana unaona hata namba haina ila ikikamilika kila kitu itakuwa barabarani soon.”

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad