Masanja: Uchungaji Si Mzaha, Afunguka Haya

MCHEKESHAJI wa kundi la Orijino Komedi, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’, amewataka wanaomtuhumu kwamba anatumia tiketi ya uchungaji kama njia ya kujiingizia kipato wajaribu kazi hiyo wataona malipo yake.

Aliongeza kuwa uchungaji ni wito na siyo kazi, pia uchekeshaji ni ajira yake, hivyo hawezi kuacha uchekeshaji kwa sababu ya uchungaji kwa kuwa hakiuki miiko ya uchungaji.

“Eti wanasema uchungaji na siasa wapi na wapi, mbona kuna chama cha siasa kimojawapo mgombea wao wa urais ameletwa na mchungaji lakini kwangu ndiyo siyo sawa? Anayedhani uchungaji ni dili, ajaribu aone kama hajatoka majipu kama Ayubu,” alieleza Masanja, alipokuwa katika moja ya mikutano ya kampeni ya kisiasa alipoalikwa na Chama Cha Mapinduzi.

Chanzo: Mtanzania
Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kwenda kule kibaraka wewe
    Mtatumwa sana
    Mbona hata mashehe huipigia debe CCM
    Lowassa it's our choice

    ReplyDelete
  2. Anatafuta ulaji hakuna lolote..maisha ya siku hizi kila mtu anaweza kuwa mchungaji ali mradi anajua kukariri biblia.. hapo ulaji atapata...

    ReplyDelete
  3. kariri na wewe tuone kama utakua mchungaji na utapata malipo

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad