Polisi Wakimbilia Kumuokoa Mtoto aliyekua Kafungiwa kwenye Gari na Kupigwa na Butwaa



Team ya polisi huko Oakland, California walipigiwa simu na wananchi baada ya mtoto mchanga kuonekana akiwa kaachwa kwenye gari na madirisha yakiwa yamefungwa. Ili kumuokoa mtoto huyo walivunja dirisha la gari hiyo kwa haraka na huku wakiwa tayari na madaktari wakisubiri kuokoa maisha ya mtoto huyo mchanga.

Baada ya kuingia kwenye gari, hawakuamini macho yao.



Huwezi kuamini hakua mtoto bali alikua mdoli, mdoli aliyefanana na mtoto kabisa. Mapolisi hao walimuelewa raia aliyewapigia kwasababu hata wao walipomuona walishangaa sana.

Top Post Ad

Below Post Ad