Shamsa Ford: Nataka Mabadiliko.....Siwezi Kujidhalilisha Kufuata Fedha CCM

Staa wa  filamu ya Chausiku, Shamsa Ford amesema hatobadilisha msimamo wake wa kushabikia vyama vya upinzani kwa kulaghaiwa na wasanii wachache kwa maslahi yao binafsi .

Shamsa amesema hayupo tayari kufuata maamuzi ya watu wengine hata kwa lundo la fedha kwani  kufanya hivyo  ni kujidhalilisha .

Mimi nitabaki huku kwa kuwa nahitaji mabadiliko,kila siku wasanii tunalia tukidai tunaibiwa na hakuna utekelezaji na matokeo yake tunapewa ahadi zisizoisha.”Amesema Shamsa

Aidha , Shamsa Ford aliwataka mashabiki kuwaona kama watu wakawaida kwani baada ya siasa maisha yataendelea kama zamani.

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. hapo shamsa.Kaza kamba mama .mabadiliko .acha hao wanaongwa nakusahau kuwa hizo pesa ni jasho la watanzania ambao wanawasaliti

    ReplyDelete
  2. umenena dada, ndiyo maana tunakupenda, pesa nini bana, zinatafutwa siyo utu! utakuta mtu anapoteza utu wake sababu tu ya NJAAA!!

    ReplyDelete
  3. Weeee atathubutu kuja CCM,si atakuta katupiwa mizigo yake nje.
    Baki hukohuko UKAWA dadangu, linda ndoa yako.Mrs Nay?????????

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad