Dk Kitila Mkumbo Atoa Neno Baada ya Ushindi wa Magufuli..“Huu Uchaguzi Ulikuwa ni Tofauti na ile ya Miaka iliyopita...."

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Ualimu cha Chang’ombe (Duce), Dk Kitila Mkumbo alisema Dk Magufuli alipitia njia ngumu kupata mafanikio hayo.
“Amepambana na ushindani mkubwa,” alisema Dk Kitila aliyeongea na Mwananchi baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo ya uchaguzi ambao ulikuwa ni vita baina ya Dk Magufuli na Lowassa, ambaye ni Waziri Mkuu wa kwanza kukihama chama tawala na kugombea urais kwa tiketi ya upinzani
“Huu uchaguzi ulikuwa ni tofauti na ile ya miaka iliyopita. Sasa ana kazi kubwa ya kutuunganisha ili tuwe wamoja tushiriki kufanya kazi kwa maendeleo ya nchi yetu.”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad