Facts: Kwanini Magufuli Kamshinda Lowassa Ndani na Nje ya CCM

Mgombea wa CCM ametumia masaa mengi kufafanua ilani ya Chama Chake.

Mgombea wa CCM amewafikia mamilioni ya watanzania katika vijiji na wilaya zao na pia kwa kupitia media mbalimbali.

Mgombea wa CCM amesaidiwa vyema na Mgombea Mwenza katika kufika majimbo yote Tanzania na kuamsha matumaini ya kina mama na watoto...hajaenda bar kumwaga sera za kilevi!!

Mgombea wa CCM ameibeba ajenda ya taifa ya kupambana na ufisadi na pia amerejesha ajenda ya kitaifa kwamba nchi hii si ya kibepari bali ni ya wakulima na wafanyakazi.

Mgombea wa CCM ameongelea ahadi zake kwa kuangalia vision 2025 na sio ahadi za kutoa wafungwa magerezani.

Mgombea wa CCM ameligusia suala nyeti la Migogoro ya Ardhi iliyosababishwa na mabwanyenye yanayogombea urais kupitia UKAWA.

Mgombea wa CCM amewaombea kura vizuri Wabunge na Madiwani wa CCM na hivyo kuacha hazina ya watu watakaoelimisha wananchi juu ya kumchagua hata baada ya kumaliza kampeni za majimbo.

Mgombea wa CCM ameomba na kusisitiza kuomba kura kwa wananchi wote kutoka vyama vyote.

Mgombea wa CCM yuko na anaonekana kuwa mkakamavu kuweza kuwa Amir jeshi Mkuu.

Mgombea wa CCM ndiye Mgombea pekee aliyeiongelea amani ya mama Tanzania mara nyingi kuliko mgombea yoyote.

Mgombea wa CCM ndiye mgombea pekee aliyefanya kazi kama waziri na kazi yake kugusa kila wilaya Tanzania hii.

Mgombea wa CCM ndiye mgombea pekee aliyeeleza kwa ufasaha kwamba muelekeo wa kiuchumi wa Tanzania ni kutoka tulipo na kuingia kwenye uchumi wa viwanda.

Mgombea wa CCM ndiye mgombea pekee aliyeweza kufurahi na audiance yake ikiwa ni pamoja na kucheza,kupiga pushups na kupiga drums.

Ni mgombea pekee anayeamini katika kazi kuwa msingi wa kujinasua na umasikini.

Mgombea wa CCM ndiye mgombea pekee aliyekiri changamoto za serikali na chama chake na hivyo kuahidi kuzitatua...yuko honest.

Mgombea wa ccm ndiye mgombea pekee alionesha kuwa hatobabaishwa au kupelekwapelekwa na watakaomzunguka...alionesha ukali palipostahili kukemewa.

Mgombea wa CCM hajatumia fedha kuhonga washabiki.

Mgombea wa CCM ametumia muda wa miezi miwili tu kuiteka jamii kwa hoja na msisimko.

Mgombea wa CCM amevunja makundi yaliyoitafuna CCM kwa miongo kadhaa.

Ameweza kuzipasua ngome za Chadema kama Arusha mjini,Moshi na Hai.

Mgombea wa CCM anawaacha mbali sana wasindikizaji katika kinyanga'nyiro hiki.


#hapakazitu

Top Post Ad

Below Post Ad