Hatimaye Mama Maria Nyerere Ampigia Kampeni Magufuli

CCM tayari wameshatengeneza video ya mama Maria Nyerere akiwaomba akina mama wotewampigie kura Magufuli. Video hii iko inasambaa Whatsup.

Kaongea mengi kuwa ni mchapa kazi na Mwadilifu. Swali langu kwa bibi angu mama Maria, ikiwa CCM itashindwa, heshima yote tunayokupa sisi wananchi itakuwaje? Maana yake wote watakaoongoza rohoni mwao watakuwa wanajua kabisa hukuwapenda ila basi.

Ni bora mama ungebaki neutral. Na ungejikita kutuombea tuchaguane kwa Amani ili uendeleee kuwa Mama wa Taifa.

Ila tutasamehe tukiamini imekulazimu, maana hakuna jinsi

Top Post Ad

Below Post Ad