Kesho ni Siku ya Mwisho ZEC Kumtangaza Rais..Nini Hatima ya Zanzibar Kuanzia Jumatatu

Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar itakapofika November 2 madaraka ya rais aliyepo yatakoma labda baraza la wawakilishi liitishwe kutengua kifungu hicho.

Wakati huo CUF imetoa hadi kesho ZEC wawe wametengua tamko la M/kiti wao na kuendelea kuhakiki majimbo 14 yaliyobaki vinginevyo watawaachia wananchi kudai haki yao wenyewe.

Nini hatima ya Zanzibar kuanzia jumatatu, je Sheni ataendelea kuheshimiwa kama rais au atatafutwa kiongozi wa mpito kipindi cha kusubiri uchaguzi mwingine.

Endapo Dr. Shein ataendelea na madaraka ataaminika vipi kuendelea kupanga uchaguzi wa marudio wakati yeye ni mmoja wa washindani wanaolalamikiwa?

Nawasilisha.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad