Mahaba ya Wana Dar Yamfanya Wizkid Aahidi Show ya Bure, Lakini Imeshindikana..Sababu Hizi Hapa

Wizkid
Mapokezi na mapenzi aliyoyapata Wizkid jijini Dar es Salaam yamemfanye avunje safari yake leo kurudi Lagos, na kuahidi show ya bure Jumapili hii.

Wizkid alioneshwa kushangazwa na shangwe za mashabiki hao, hali iliyofanya afanye show kwa muda mrefu zaidi. Alisema hakuwahi kukutana na mashabibi wenye upendo kuwazidi Watanzania.

“Ilikuwa niondoke lakini sitaondaka na kesho natafuta sehemu nikutane tena na nyie, tufanye concept ya bure,” alisema Wizkid.

Nimefurahi sana kuona hali hii. Tanzania mna upendo wa kweli. Tuendelee kuwa pamoja nami kwenye Twitter na Instagram ili tujue tunakutana katika ukumbi gani,” alisema.

Hata hivyo Jumapili hii Wizkid alitangaza kuwa ameshindwa kupata kibali cha kufanya show ya bure lakini amedai atarajea December kwenye Fiesta.

Last night in Dar es Salaam, Tanzania!! Had to jump on the speakers to be close to my people! Love u all. Unfortunately, we couldn’t get the permit to do the free concert today but I’m coming back in December! Fiesta moves!!!!! Yaaaaa,” ameandika kwenye Instagram.

Pia aliipongeza Tanzania kumaliza uchaguzi salama.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad