Mwanamuziki Cassim Mganga Amchana Babu Tale... Adai Hakuwa ‘Kiongozi Bora’ Wakati Yupo Tip Top Kiasi Alijihisi Mtoto wa Kambo

Cassim Mganga
Cassim Mganga amezungumza kwa kwanza sababu ya kuondoka Tip Top Connection ambapo amemtuhumu Babu Tale kuwa hakuwa kiongozi mzuri kwake.

Cassim alikiambia kipindi cha Mkasi kuwa hakufurahishwa na maisha aliyoishi Tip Tip ndio maana aliamua kuondoka.

Toka nimeondoka Tip Top Tale hajawahi kuniletea deal hata moja,” alisema.

Kwenye familia yoyote hakukosi migogoro, mzazi usipokuwa strong watoto wanapoteza direction. Nimeishi muda mrefu Tip Top, nimekosea nimekosewa lakini ilikuwa ni sehemu ya maisha kama family. Naomba nifunge, Tale hakuwa baba bora. Baba lazima umsikilize kila mtoto, kwahiyo mimi nilikuwa najiona mtoto wa kambo. Sasa kwa nini niendelee kuishi? Lakini kutoka kwangu bado kulisababisha vitu vingi sana na ninachokiona ni kwa sababu ya uwezo wangu. Walitamani kuona mtu kama Cassim aendelee kuwepo, hata mimi nilitamani kuendelea kuwepo kwa sababu kazi zilikuwa rahisi sana.”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad