UKAWA Wapinga Hotuba ya Rais Magufuli bila Matokeo ya Zanzibar.....Wapinga Dk Shein kuingia bungeni

Vyama vinavyounda Ukawa wamesema wamemwandikia Spika wa Bunge, Job Ndugai barua kutaka kujua uhalali wa Rais John Magufuli kuhutubia Bunge bila matokeo Rais wa Zanzibar kujulikana.

Katika mkutano wao na waandishi leo, wamesema kuwa hawatakubali Katiba ivunjwe kwa kumruhusu Dk Shein kuingia bungeni wakati muda wake wa kushika madaraka ulishapita.

Katika hatua nyingine, Umoja huo umesema wabunge wa kambi ya upinzani bungeni wamekubaliana kuchanga kila mmoja Sh 300,000 kwa ajili ya kuchangia familia ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Geita, Alphonce Mawazo.

Uamuzi huo umetangazwa na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe kwenye mkutano wa waandishi wa habari bungeni baada ya kikao cha wabunge wote wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Pia wamekubaliana Jumamosi ya Novemba 21, wataenda wabunge wote kuungana na viongozi wengine wa kitaifa kumzika marehemu Mawazo.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. KUSUSIA VIKAO NA KUPINGA KILA KITU, hiyo hasa ndio kazi ya upinzani hapa Tanzania, na ndio kazi ilowapeleka hapo bungeni, na ndio sababu mkachaguliwa, nyinyi ni KUPINGA, KUPINGA ......hahahaha HAPA KAZI TU

    ReplyDelete
  2. PINGENI NA HIZO POSHO PIA NA JINSI MNAVYOKOKOTOA BAADA YA BUNGE.MIAKA 5 MILLION MIA 230,WENGINE NAWASIKIA WAKO BUNGENI TANGU NAZALIWA,MIE
    BABANGU MIAKA 39 KAZINI LAKINI KASTAAFU HATA MILLION 50 HAZIFAFIKA.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad