CHADEMA Yaionya CCM Umeya Dar es Salaam

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemteua diwani wa Ubungo, Isaya Charles kugombea nafasi ya Meya wa jiji la Dar es Salaam, na kuitahadharisha CCM hakitakubali kuchezewa rafu katika uchaguzi huo.

Aidha, Chadema imemtangaza diwani wa Ubungo, Boniface Jakob kuwa mgombea wa nafasi ya Meya wa Kinondoni na diwani wa kata ya Bonyokwa, Charles Kuyeko kugombea umeya wa Ilala.

Uteuzi huo ulitangazwa jana jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu Chadema (Zanzibar), Salim Mwalimu wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Majina hayo yaliteuliwa kwa ushirikiano ndani ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), alisema.

Mwalimu alisema wanatarajia kuona uchaguzi huo ukifanyika kwa amani na utulivu bila kuwepo na ubadilishwaji wa matokeo, kwa kuwa kuna mbinu chafu zinazofanywa na CCM sasa.

Alisema katika Halmashauri za Ilala na Kinondoni Chadema inaongoza kuwa na madiwani wengi lakini cha kushangaza CCM imekuwa haitaki kuyakubali matokeo hayo na kutaka kuyabadilisha.

"Kwa mujibu wa taratibu zilivyo ni kwamba Hamashauri yenye madiwani wengi ni kuwa chama hicho huchukua ushindi lakini hawa wenzetu CCM wamekuwa hawataki," alisema.

"Mfano mzuri katika Wilaya ya Temeke madiwani ni wengi wa CCM tumekubali huo ushindi kwa kuwa ni kweli wametuzidi.

"Kinondoni na Ilala hawataki umeya uchukuliwe na Chadema licha ya kuwa na madiwani wengi na sisi hatuwezi kukubali njama za wazi zinazofanywa na CCM.
"Na hata meya wa jiji lazima atoke Chadema kwa kuwa katika mkoa wa Dar es Salaam tunaongoza kuwa na madiwani wengi."

Mwalimu alisema ameshangazwa na kitendo cha CCM kwenda Zanzibar kuchukua wabunge kwa ajili ya kupigia kura Kinondoni.

Alisema kitendo cha wabunge hao kukubali jambo hilo ambalo ni la aibu katika jamii inayowazunguka ni sawa na kuwazalilisha Wazanzibari kuwa hawajasoma.

"Unakubalije kubebwa kutoka Zanzibar kuja kupigia kura meya wa Kinondoni! Hivi kabisa mwenyekiti wa chama cha CCM anakubali hii aibu ya wazi wazi isiyohitaji propaganda ya kuleta majeshi Zanzibar" "Hilo jambo tutalipinga kwa nguvu zote."

Pia Mwalimu ameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kuhakikisha inamaliza changamoto zote zilizojitokeza katika viti maalum vya udiwani.

"Huko Kelwa tumeshinda viti vya udiwani 13 na CCM wameshinda 11 katika mgawanyo wa viti maalum Chadema wamepatiwa viti vinne na CCM imepatiwa vitano,? alisema.

"Hapa tumeitaka NEC itueleze huo mgawanyo umegawanywa vipi" Tumeenda kuwauliza wanatueleza Mkurugenzi hawampati kwenye simu ili athibitishe ni nani mwenye madiwani wengi. Eti mkurugenzi hapatikani na mwezi umeshapita."

CHANZO: NIPASHE
Tags

Post a Comment

10 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. mikwara ya nin sasa hamjiamini
    waonye madiwani wenu wasije uza nafasi tuu kama mlivyouza urais kwa luwasaa
    manake ukawa wote ni watu wa dili

    ReplyDelete
    Replies
    1. Koma wewe hata CCM kuna dili
      No maana Msoga haiguswi
      Punda wewe Kuma wewe

      Delete
    2. Tatizo la mipaka ndio hilo,kinachokufanya utukane nini.Mwangalie kwanza kubwa zima aibu huna ndio tatizo la kutoenda kumbi la kienyeji.Jiheshimu

      Delete
  2. CCM AKILI ZAO ZIMESHEHENI UOVU NA UCHAFU TUZUNGUMZIE MFANO HAI MANISPAA YA ARUSHA. KULE KWENYE UCHAGUZI MKUU WALISHINDWA VIBAYA SANA DIWANI WA CCM NI MMOJA TUU,NARUDIA MMOJA-1-,WAKATI MADIWANI WA CHADEMA NI THERATHINI NA TATU-33-SASA ONA MAAJABU YA UZANDIKI WA CCM, KWENYE KUGOMBEA UMEYA HUYU DIWANI WA CCM ALIJAZA FOMU NA ALIGOMBEA NA AKAPATA KURA MOJA,YAANI YA KWAKE NADHANI KAMA ULIKUA HUIJUI CCM,BASI ITAZAME HAPO .WAMEJAA HILA,WANAPENDA FUJO,WEZI WAKUBWA,HAWAKUBALI KUSHINDWA HIVYO ANAVYOTAHADHARISHA MWALIMU, NAIBU KATIBU MKUU WA CHADEMA NI KWELI,NI SAHIHI,UKAWA MUWE MACHO ASILIMIA MIA MOJA-100%-HII NI VITA CCM SI WAUNGWANA HATA CHEMBE.WEZI,WEZI,WEZI,WEZI,WEZI WAKUBWA.

    ReplyDelete
  3. ibeni tuu ccm hakuna kuwapa nafasi hao wahuni wa ukawa hawana mpya fujoo tuu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Nasema hivi,kama meya wa Dar akitoka Chadema mje mumchukue mume wangu pamoja na mali zake zote!

      Delete
  4. ukawa hawataeza kwenda na kasi ya magufuli ukawa acheni tuu meya atoke ccm ili aende sambamba na kasi ya magufuli
    tanzania kwanza vyama badae ukawa tulieni kidogo sasa tumewachoka na kelele zenu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kuna wewe Kwani Magufuli Nani
      Nyoko wewesianaiga ilanizetu
      Magufuli ji chadema moyoni

      Delete
    2. mna ilani nyie wahuni magufuli kidume ndo maana hakukimbia chama kama huyo mamvi wenu
      magufuli anajenga chama sasa sio nyie wahuni midomo yenu imejaa matusi hata aibu huoni na Mungu akusamehe bure hujui chochote unakurupuka kwa mitusi utatukana mpaka mama zako boya wewe magufuli ni wa ccm sio wahuni wa ukawa

      Delete
  5. Koma mwana kukoma
    Magufuli ni UKAWA damu
    Wakukaya huyo
    Fyuuuuuuu
    Unafikiri Magufuli anahonga vyeo
    Mtausaga mtama

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad