Harmonize: ‘Directors’ wa Video Kutoka South Africa, Wanatuheshimu Sana Wasanii Kutoka Tanzania.

Chipukizi wa Bongo flava anayeunguruma poa na hit yake ‘Aiyola’, Harmonize amesema waongozaji wa video za muziki kutoka Afrika kusini huwa wanaonesha heshima ya hali ya juu wanapokutana na wasanii kutoka Tanzania.

Akifunguka mbele ya kipaza sauti cha Timesfm.co.tz, Mkali huyo ambaye jina lake halisi ni Rajab amedai sababu kubwa ya kupewa heshima ni kwa kuwa mziki wetu ni wa pili kwa ukubwa Barani Afrika ukiwatoa Nigeria.

“Labda mi niseme kitu kimoja” alisema “Directors wa kule(Afrika kusini) wanajua kabisa ili uweze kuhit Afrika mashariki ni lazima utusue Tanzania, na hilo liko wazi sisi ni wa pili kimuziki Afrika na tunaushindani mkubwa na Nigeria tu.

huduma huwa zinakuwa nzuri kiukweli, wanatu treat poa yani hadi unaona heshima unayopata” alimaliza.

Nafasi za Kazi Kutoka Magazetini leo

Bonyeza www.ajirayako.com
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. umeyajua yote hayo kwa nyimbo moja tu? huyu dogo hana muda mrefu kwenye ummarufu maana anjifanya mjuaji mno.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad