Kasi ya Magufuli Yaikumba Clouds FM...Mwaka Huu Tamasha la Fiesta Halitafanyika

Mkurugenzi wa Clouds Media Group ambao ni waandaaji wa tamasha la Fiesta, Ruge Mutahaba amesema kuwa tamasha hilo halitakuwepo mwaka huu.

Amesema wameamua kuahirisha kufanya tamasha hilo mwaka huu kutokana na ufinyu wa muda uliobaki hasa baada ya kupisha kipindi cha uchaguzi.

“Tulijua tukimaliza kampeni tutafanya kwa mikoa michache lakini tumeona kwamba hakuna kitu kizuri kama kumsupport mheshimiwa Magufuli , hebu sasa hivi turudi kwanza tutulie tuache hii amsha amsha aliyoanza nayo ianze kufanya kazi tujipange kwaajili ya Fiesta 15 ambayo itafanyika mwaka kesho,” Ruge aliiambia XXL ya Clouds Fm.

“Tutakuwa tunafikisha miaka 15 ya Fiesta na nina uhakika itakuwa na ukubwa inayostahili kuliko kufanya kitu kidogo mwaka huu. Tumeona tuache mwaka kesho mikoa 15, miaka 15 ya Fiesta itakuwa kubwa zaidi. Hapa Kazi imebidi iivae Fiesta pia,” alisema.

Nafasi za Kazi
Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Tushaona fiesta wakati WA kampeni mtabadilisha nini wakati wasanii Ni wale wale tuu

    ReplyDelete
  2. Mmmmmh!! Mnawaletaga kinyemela nini wasanii Na kurukaruka kodi. Haya wasanii mjipange nanyi mlipwe vizur

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad